IQNA

Umoja wa Waislamu

Ayatullah Al-Hakim wa Iraq akutana Sheikh Mkuu wa Al Azhar mjini Cairo

22:28 - May 30, 2023
Habari ID: 3477073
TEHRAN (IQNA) - Ayatullah Ammar al-Hakim, kiongozi wa Harakati ya Al-Hikma (Hekima) ya Iraq, amekutana na mkuu wa Kituo cha Kiislamu cha Al-Azhar cha Misri Sheikh Ahmed al-Tayyib.

Maafisa wengine kadhaa kutoka pande hizo mbili pia walikuwepo kwenye mkutano huo. Vyombo vya habari vya Iraq vimeelezea mkutano huo wa Jumatatu asubuhi kama wa kufurahisha. Akiongoza ujumbe wa ngazi za juu, Ayatullah Al-Hakim amesafiri hadi mji mkuu wa Misri kwa mazungumzo na maafisa wa nchi hiyo ya Kaskazini mwa Afrika. Ujumbe wa Iraq pia ulikutana na rais na waziri wa mambo ya nje wa Misri siku ya Jumapili.
Wakati wa mazungumzo hayo, Ayatullah Al-Hakim alisisitiza haja ya kudumisha mwelekeo chanya wa sasa wa mahusiano ya kikanda ili kuimarisha usalama na utulivu wa kikanda. Pia alionya kuhusu changamoto ambazo mkoa huo utakabiliana nazo endapo hali hii itadhoofika.

Iraq’s Al-Hakim, Al-Azhar Chief Meet in Cairo

4144387

 

captcha