IQNA

Msomi wa Kuwait

Kususia India kiuchumi kutaifanya ijutie kuutusi Uislamu

15:13 - July 03, 2022
Habari ID: 3475455
TEHRAN (IQNA) – Msomi wa chuo kikuu nchini Kuwait alisema vikwazo vya kiuchumi ni mojawapo ya nguvu kuu za Waislamu katika kukabiliana na serikali zinazounga mkono chuki dhidi ya Uislamu.

Abdullah Ahmed Safar Ibil aliiambia Shirika la Habari za Qur'ani la Kimataifa (IQNA) katika mahojiano kwamba nchi zinahitaji ukuaji wa uchumi, ambao ni muhimu sana kwa serikali.

Kama India haitaacha kuwabagua Waislamu na itaendelea kuruhusu kuvunjiwa heshima matakatifu ya Kiislamu, nchi za Kiislamu zinapaswa kuiwekea vikwazo, amesema.

Haya hapa mahaojiano ya IQNA  mwanazuoni huyo wa Kuwait

Swali: Ni nini kilicho nyuma ya matamshi ya matusi dhidi ya Mtume Muhammad SAW ambayo yametolewa na vinara wa chama tawala nchini India?

Jibu: Uislamu daima umekuwa ukikabiliwa na mashambulizi yenye lengo la kudhoofisha na kudharau matukufu yake. Wale wanaovunjia heshima matukufu ya Kiislamu nchini India au baadhi ya nchi za Magharibi wanataka kuidhalilisha dini ambayo mawazo yake yameenea katika upeo mkubwa na ina mafungamano mazuri na imani nyinginezo. Tukifuatilia vyanzo vya habari, tutatambua kwamba katika miaka ya hivi karibuni, Uislamu umeshuhudia ukuaji mkubwa zaidi (kati ya dini nyingine). Hii ni dini ya kila mahali na nyakati zote lakini wale wanaoudharau Uislamu hawataki kuona kukua kwake na hivyo hukimbilia kuvunjia heshima matukufu yake.

Kuhusu yanayojiri dhidi ya Waislamu nchini India, kunyanyaswa kwa Waislamu, hasa wasichana wa Kiislamu ambao wamezuiwa kuingia katika baadhi ya vyuo vikuu kwa kuvaa Hijabu, ni jambo la kusikitisha.

Tofauti zinapaswa kuheshimiwa, kama vile Waislamu, kwa mujibu wa mafundisho ya Qur'ani Tukufu na Sunna za Mtukufu Mtume (SAW), wanavyowatendea vyema wafuasi wa imani nyinginezo.

Swali: Je, Muislamu anapaswa kuchukua hatua gani  anapotukanwa Mtukufu Mtume (SAW)?

Jibu: Tumeona video nyingi za jinsi polisi wa India wanavyowashambulia kikatili waandamanaji Waislamu, jambo ambalo ni ishara ya ukandamizaji dhidi ya Waislamu nchini humo. Ili kukabiliana na hili, tunapaswa kuchukua hatua za kiuchumi.

Mara nyingi vitendo hivyo vya kuvunjia heshima matukufu ya Kiislamu vinalenga kuona jinsi Waislamu watakavyojibu au ni hatua gani watakazochukua. Ikiwa kuna majibu yenye nguvu, hawatapata ujasiri wa kuendeleza maovyo yao

Swali: Matamshi ya matusi ya maafisa wa India yalizua hasira kubwa katika mataifa ya Kiislamu na baadhi yao waliwaita mabalozi wa India kuwasilisha malalamiko rasmi. Je, majibu haya yanafaa?

Jibu: Kuhusu matamshi ya matusi ya hivi majuzi nchini India, kulikuwa hatua zilizochukuliwa katika nchi za Kiislamu na Kiarabu, huko Kuwait, Qatar, Afghanistan, Malaysia, Iran, Libya na Pakistan, miongoni mwa nyingine, zikiwaita mabalozi wa India. Hatua hizi zililazimisha New Delhi kuachana na baadhi ya matamshi.

Kwa kweli, nchi za Kiislamu zina uhusiano muhimu na India na baadhi ya asilimia 15 ya biashara ya India iko na nchi za Ghuba ya Uajemi. Pia kuna takriban raia milioni kumi wa India wanaofanya kazi katika nchi za Kiarabu za  Ghuba ya Uajemi. Ikiwa nchi za Kiislamu na Kiarabu zitachukua msimamo mkali, itaifanya India kufikiria upya tabia yake.

Serikali ya New Delhi na wanachama wa chama tawala cha Bharatiya Janata Party (BJP) wanazungumza kuhusu kuheshimu haki za walio wachache na kudumisha uvumilivu, lakini tunaona ukandamizaji wa kimfumo wa Wahindu dhidi ya Waislamu na vitendo vyao vya misimamo mikali dhidi ya Waislamu kwa msaada wa vikosi vya polisi vya India.

Economic Boycott Would Make India Regret Insulting Islam, Kuwaiti Scholar Says

Swali: India inajulikana kama nchi yenye wingi wa kikaumu na kidini na Waislamu wana historia ndefu katika nchi hii. Kwa nini kumekuwa na visa vya dhuluma na dhuluma dhidi ya Waislamu nchini India?

Jibu: Baadhi ya haya yana mizizi katika chuki na ubaguzi wa rangi. Bila shaka tunayoyaona India kuhusiana na ubaguzi dhidi ya Waislamu yamekuwepo kwa muda mrefu.

Uislamu umekuwa na nafasi nzuri sana katika maendeleo ya India na taifa la India, lakini pale wasiokuwa Waislamu walipokuwa watawala katika nchi hiyo, tumeshuhudia misimamo mikali na dhulma dhidi ya Waislamu.

Swali: Tumeona kile kilichotokea kwa Waislamu (wa Rohingya) nchini Myanmar. Unafikiri nchi na taasisi za Kiislamu na Kiarabu zinaweza kufanya nini kuzuia ukatili huo dhidi ya Waislamu?

Jibu: Suala la kiuchumi ni muhimu kwa sababu serikali zote zinatafuta kukuza uchumi wao ili mataifa yao yaishi kwa amani na ustawi.

Nchi inapowakandamiza Waislamu, kama ilivyotokea Myanmar, nchi hiyo inapaswa kususiwa ili ilazimike kubadili tabia yake. Kususia kiuchumi kunaweza kuwa miongoni mwa nyenzo zenye nguvu zaidi kuzifanya nchi ziache kuwakandamiza Waislamu wasio na ulinzi.

Habari zinazohusiana
Kishikizo: waislamu india bjp
captcha